Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 09/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 09/2024

SIKU 1 YA 30

Kukamatwa kwa Yesu na hatimaye kuuawa halikuwa jambo lililotokana na uhodari wa wakuu wa makuhani na viongozi wengine. Yesu mwenyewe aliyajua yote yaliyompata, na hata akawaambia wanafunzi wake ili wasije wakafadhaika na kukata tamaa wakati wa kifo chake. Habari hii inatupa ushuhuda kwamba, mpango mzima wa kuja kwa Yesu duniani, kufa na hata kufufuka kwake, uliratibiwa mbinguni. Hatuna sababu ya mashaka kuhusu ukombozi mkamilifu pale msalabani, kwani ni mpango wa Mungu.

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2024

Soma Biblia Kila Siku 09/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Tisa pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz

Mipangilio yanayo husiana