Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2025

SIKU 15 YA 31

Hezekia ni mmoja wa wafalme waaminifu wa Yuda. Alifanya kazi kubwa ya kukumbukwa ya kuondoa ibada ya miungu na kutakasa hekalu la Yerusalemu. Hata hivyo alijua kuwa utawala wake haukuwa safi wakati wote. Mawimbi ya uovu yangeleta maangamizi. Alijua kwamba Mungu ndiye aliyeingilia kati kwa muujiza wake na kuliokoa taifa dhidi ya maadui zake. Alipokufa, taifa lilitumbukia katika maisha ya uovu na dhambi. Manase, mtoto wake Hezekia, hakufuata mfano wa babaye. Unajifunza nini kutoka kwa Hezekia?

siku 14siku 16

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2025

Soma Biblia Kila Siku 03/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko, 1 Nyakati na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz