Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 03/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 03/2025

SIKU 12 YA 31

Maisha ni kama safari. Hutokea tunapita katika misukosuko na shida mbalimbali, kama vile vita, magonjwa, kukataliwa n.k. Mambo ya jinsi hiyo hufanya watu kujiuliza, Ni laana? Je, tumekataliwa na Mungu? Bila kujali mtu anavyojibu swali hilo, zaburi hii inatia moyo. Israeli waliipitia hali kama hiyo ya vita kila upande, wakajisikia kuzama. Lakini haikuwazuia kumwomba Mungu awasaidie, wala haikumzuia Mungu kuwaopoa:Umewapa wakuogopao bendera, ili itwekwe kwa ajili ya kweli. Ili wapenzi wako waopolewe, uokoe kwa mkono wako wa kuume, utuitikie.Mungu ametupa msalaba kama bendera ili tujue mahali pa kukimbilia na kuokoka.

siku 11siku 13

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2025

Soma Biblia Kila Siku 03/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko, 1 Nyakati na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz