Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 05/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

SIKU 28 YA 31

Mungu anamwagiza Musa aandae vibao vipya kwa ajili ya kuandika amri kumi za Mungu. Mungu alipomwumba mwanadamu kwa mfano wake aliiandika sheria katika moyo wake. Lakini wenye dhambi wanahitaji kuwa nayo kwenye ‘vibao’. Ni pale tu tunaposamehewa na kuingia katika agano jipya la Yesu Kristo kwamba ‘shingo’ yetu ngumu inaondolewa na tunapewa moyo mpya wenye sheria yake kuandikwa ndani yake ambao hupenda mapenzi ya Mungu. Mungu anavyojitambulisha inamsukuma Musa kuwaombea watu kwa mara nyingine.

siku 27siku 29

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

Mipango inayo husiana