Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 05/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

SIKU 24 YA 31

Mungu anajua na anaona hatua zote za kumwasi anazoziendea mtu, na uovu huu wa kumwasi una adhabu yake. Unaharibu uhusiano wako na Mungu na pia wewe mwenyewe unayeufanya, maana Mungu havumilii uovu wa aina yoyote. Lakini katikati ya uovu huu, Mungu anainua watumishi wake, kama vile Musa, wanaomsihi na kumkumbusha Mungu juu ya ahadi zake. Katika m.13 Musa anamwomba hivi:Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele. Musa anawaombea watu kwa Mungu ili wasamehewe dhambi na makosa yao. Neema ya Mungu itusaidie kukataa ubaya na kurejea kwa Mungu ikiwa tumemkosea.

siku 23siku 25

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

Mipango inayo husiana