Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 05/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

SIKU 21 YA 31

Musa anaambiwa jinsi ya kuandaa vifaa vitakavyotumika kwenye ibada na kwa ajili ya kuweka wakfu watumishi watakaosimamia huduma hizo. Agizo la kutumia manukato hulenga kuonyesha heshima na utii kwa Mungu. Ni kama maombi ya kuwainua watu kwa Mungu. Kimsingi, kuhani na mtu mmoja mmoja wanaitwa na kutiwa moyo ili waishi maisha yenye kujaa roho ya kumcha na kumtegemea Mungu. Hivyo maisha yao yatatoa harufi nzuri kama manukato. Uchaji ni maisha yaliyojaa uhusiano wa kweli na Mungu.Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu(Rum 12:1-2).

siku 20siku 22

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

Mipango inayo husiana