Soma Biblia Kila Siku 11Mfano

Baada ya kila fundisho Paulo anauliza swali la udadisi ambalo anajua Wayahudi wangeuliza. Leo anaelezea mambo ambayo yanapitaufahamu wa binadamu: Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi (m.20)? Kwa hiyo jambo muhimu kwa Paulo si kuiridhisha akili ya binadamu kwa kila jambo. Bali la muhimu zaidi ni kuonyesha msingi wa kila fundisho katika Maandiko Matakatifu(angalia m.15 na 17 kuhusu anavyothibitisha aliyoandika:Maana [Mungu]amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. … Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote). Fundisho: Kuokoka kunategemea neema ya Mungu tu (m.16: Si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu)!
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 11 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Warumi na 1 Samweli.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku 02/20

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021
