Soma Biblia Kila Siku/ Aprili 2023Sample
Musa alionesha dalili ya kutoamini yeye mwenyewe, kama vile alivyokuwa na wasiwasi kuhusu imani ya Waebrania. Haijalishi hakuweza kunena au la, tabia yake ilionesha kujitafutia udhuru tu, na jambo hili halikumpendeza Mungu, kwa sababu Mungu anapotuita ndiye pia anayetupa uwezo wote tunaohitaji kuitika, ukiwepo wa kuzungumza, kuona na kufikiri. Kama matokeo ya malalamiko ya Musa, Mungu alimchagua Haruni, kaka yake Musa, ili awe msemaji wake. Udhaifu wako si kigezo cha kutomtumikia Mungu.
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku/Aprili 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Yohana, Mithali na Kutoka. Karibu kujiunga na mpango huu bure
More