Soma Biblia Kila Siku 03/2025Mfano

Itikio la Daudi juu ya unabii uliotolewa na Nathani linaonesha unyenyekevu wa Daudi na imani yake kwa Mungu. Jibu lake liko katika sehemu mbili: Shukrani na maombi. Shukrani kwa yale ambayo Mungu amemtendea na atakayomtendea yeye na nyumba yake. Maombi yake ni litimie neno la Mungu lililonenwa. Mpendwa, kwanza tuwe niwapokeajitukimshukuru Mungu kwa yale aliyotutendea na kuendelea kututendea. Kisha tuwewatendajitukikubali kama Daudi lile ambalo Mungu anatutaka tulitende.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko, 1 Nyakati na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz