Soma Biblia Kila Siku 03/2025Mfano

Wakati Nahashi, mfalme wa Amoni alipokufa, Daudi alipeleka salamu za rambirambi kwa Hanuni, mwanawe. Lengo la Daudi lilikuwa kuonesha kwamba alitaka kuendeleza mahusiano mazuri kati ya falme hizo mbili, lakini ujumbe wake ulitafsiriwa vibaya na wakuu wa Waamoni. Walifikiri ni wapelelezi. Kwa jinsi walivyowatendea vibaya wajumbe wa Daudi walichochea vita. Lakini hata Waamoni walipowanunua Washami wawasaidie, walishindwa. Yoabu alimwambia Abishai, nduguye:Uwe hodari, tukajitie moyo mkuu kwa ajili ya watu wetu, na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu; naye Bwana afanye yaliyo mema machoni pake(m.13). Zingatia neno hili lina maana gani kwako.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 03/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko, 1 Nyakati na Isaya. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: www.somabiblia.or.tz