Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 06/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

SIKU 9 YA 30

Mtume Paulo ni mfano mzuri wa mafundisho ya kumfuata Yesu Kristo katika mwenendo na imani. Timotheo anahimizwa kukaa katika kweli na mafundisho aliyoyapokea tangu utoto wake. Anajua ni akina nani waliomfundisha vizuri. Aliyapokea kwa watu waadilifu na wenye imani thabiti. Ni baraka kubwa kujaa Neno la Mungu tangu utotoni na kuendelea nalo hata katika uzee, kama ilivyoandikwa katika Mit 22:6:Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. Kila andiko la Biblia lina pumzi ya Mungu. Kwa hiyo lafaa kwa mafundisho, kuonya watu makosa yao, kuwaongoza na kuwaadibisha.

siku 8siku 10

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

Soma Biblia Kila Siku 06/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa sita pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Timotheo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz