Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku / Oktoba 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku / Oktoba 2023

SIKU 21 YA 31

Hata baada ya Mungu kuonyesha uweza wake, Waisraeli bado walitafuta na kuabudu miungu, na Mungu wa kweli akaudhika. Kwa hiyo Mungu alihukumu Efraimu, kabila kiongozi, na kuondoa hema ya kukutania iliyokuwa katika nchi yake:Hakuichagua kabila la Efraimu(m.67) ...akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu(m.60). Lakini uaminifu wa Mungu haubadiliki. Kwa hiyo akawainulia watu wake mtawala mwingine, mfalme Daudi, ambaye aliwaongoza kwa haki na uadilifu, akawa mfano wa Kristo Yesu:Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake(m.72). Habari hiyo itutie moyo kumrudia Mungu na kumtegemea. Mungu anaaminika!

siku 20siku 22

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku / Oktoba 2023

Soma Biblia Kila Siku /Oktoba 2023 ni mpango mzuri wa kusoma biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Oktoba pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu...

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha