Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

SIKU 2 YA 28

Katika m.16-17 Paulo anaonyesha kuwa msukumo wake wa kutaka sana kuwatembelea Wakristo wa Rumi ni Injili yenyewe. Anaeleza mwenyewe sababu, Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye. Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani. Kuijua Injili, yaani habari njema ya Yesu Kristo ni utajiri mkubwa kupita kiwango! Maana Injili ina uwezo wa kufanya jambo la ajabu ambalo hakuna kitu kingine duniani kinachoweza kulifanya, yaani kumwokoa mwanadamu! Haki ya Mungu inadhihirishwa ndani ya Injili, toka imani hata imani (m.17). Yaani kwa kuamini matendo ya wokovu ya Yesu Kristo mtu huhesabiwa kuwa mwenye haki mbele ya Mungu!

siku 1siku 3

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaid...

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

Mipangilio yanayo husiana

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha