Soma Biblia Kila Siku 9Mfano

Naftali na Asheri yanamalizia makabila yaliyopokea baraka zake Bwana kwa njia ya Musa (m.23-25). Ndipo Musa anawakumbushia tena makabila yote ukuu wa Mungu na neema yake ya ajabu, kwamba Mungu wa milele ndiye makazi yako, na mikono ya milele i chini yako (m.27). Mungu wa milele hayuko mbali, bali amesogea karibu mpaka mikono yake i katikati ya taifa la Israeli. Tena yu juu yao (m.26: Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. na juu ya mawingu katika utukufu wake) na mbele yao (m.27: Mbele yako amemsukumia mbali adui; akasema, Angamiza). Kweli kabisa, U heri, Israeli. Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na BWANA(m.29).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 9 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kumbukumbu la Torati, Warumi na Mithali
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabolimo.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Kusikia Kutoka Kwa Mungu Kila Asubuhi

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
