YouVersion Logo
Search Icon

Plan Info

Soma Biblia Kila Siku/AGOSTI 2023Sample

Soma Biblia Kila Siku/AGOSTI 2023

DAY 9 OF 31

Wayahudi walitaka kumwua Yesu.Hata nduguze hawakumwamini(m.5) wala kumpenda. Maana walimpa Yesu ushauri ambao walijua utampambanisha na Wayahudi. Swali muhimu la kujiuliza ni, “Kwa nini hao walimchukia Yesu?” Katika m.7 Yesu anasema:Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. Kwa hiyo watu wa ulimwengu huu humchukia Bwana Yesu kwa sababu anawaambia ukweli. Mimi na wewe tunapokeaje ushuhuda wake juu yetu? Tukiupokea tutachukiwa na watu wa ulimwengu huu kwa sababu wanamchukia Yesu. Lakini tuhesabu tuna heri, maana neno lake ni kweli. Tulinganishe na anachosema katika Mt 5:11-12:Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

Scripture

Day 8Day 10

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku/AGOSTI 2023

Soma Biblia Kila Siku Agosti 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu Yohana na Mithal...

More

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy