Soma Biblia Kila Siku/AGOSTI 2023Sample
Bwana Yesu alifanya ishara nyingi. Kwa ishara alizozifanya alidhihirisha kwamba Ufalme wa Mungu umefika, upo na unatenda kazi. Ni ishara hizo zilizowafanya Wayahudi waliokuwa hawamwamini Yesu kupata mashaka kama kweli huyo kristo mwingine waliyemngojea ataweza kufanya ishara zaidi ya hizi alizozifanya Yesu.Wakasema, Atakapokuja Kristo, je! Atafanya ishara nyingi zaidi kuliko hizi alizozifanya huyu? (m.31). Je, wewe unamfuata Yesu kwa kuangalia nini? Ishara tu? Kumbuka, hata bila ishara Bwana Yesu anaweza kutufanya wana wa Mungu na warithi wa uzima wa milele tukimwamini yeye.
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku Agosti 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu Yohana na Mithali. Karibu kujiunga na mpango huu.
More