Soma Biblia Kila Siku/AGOSTI 2023Sample
Je, wewe unamfahamu Yesu kuwa nani? Ni jambo muhimu sana, maana ni hatua kuelekea kumwamini Yesu. Hapo haitoshi kuwa na elimu kubwa ya dini, maana tunaona viongozi wa kiyahudi hawakumfahamu Yesu kuwa yu nani. Jambo muhimu zaidi ni kusikiliza ushuhuda wa Yesu, maana huu unatusaidia kumwamini, kama ilivyoandikwa kuhusu waliomsikiliza siku ile: Yesualipokuwa akisema hayo, wengi walimwamini(m.30). Zingatia Yesu anavyojitambulisha katika m.12, 19 na 23:Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima. ...Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui...Mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.Yaani Yesu anasema si mzawa wa Yusufu, bali ni Mwana wa Mungu. Ni juu ya ulimwengu kama Mwokozi wake. Tunapomwamini hatutakufa katika dhambi zetu!
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku Agosti 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kuelewa somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu Yohana na Mithali. Karibu kujiunga na mpango huu.
More