Soma Biblia Kila Siku 01/2025Mfano
![Soma Biblia Kila Siku 01/2025](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F54349%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Hapa twajifunza kwamba ombi la mtu si kitu kidogo kwa Yesu. Yesu aliguswa na taabu ya mtu yule, akaamua kwenda kumsaidia. Ndugu msomaji, tusikawie kumkabidhi Yesu taabu zetu tukimwomba na kumsihi atusaidie! Ila wakati mwingine inaonekana kana kwamba Yesu amechelewa kutujibu. Ndipo tunajiuliza: Je, hajatusikia au ametusahau? Ndivyo ilivyokuwa siku hiyo. Yule binti akafa kabla Yesu hajaja.Wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema, Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu?(m.35) Ila angalia jibu la Yesu:Usiogope, amini tu!(m.36). Hii itutie moyo kumtwika fadhaa zetu zote.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku 01/2025](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F54349%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku 01/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Januari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko na Ezra. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz