Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 01/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 01/2025

SIKU 13 YA 31

Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu(m.11). Yesu alitumia sana mifano alipowaeleza watu juu ya ufalme wa Mungu: [Yesu]akawafundisha mambo mengi kwa mifano, akawaambia katika mafundisho yake(m.2). Hivyo aliiweka wazi habari ya ufalme wa Mungu, haikuwa tena siri. Hata hivyo kuna wengine waliokuwa hawaelewi. Ila wanafunzi wa Yesu walitambua, maana walipokea kwaimani(m.20). Ndivyo ilivyo hata leo! Fundisho:1.Neno la Yesu lipewe umuhimu wa kwanza kwa maisha yetu yote.2.Tumsihi Yesu atufunulie maana ya neno lake kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Wanafunzi ni kielelezo kizuri: [Yesu]alipokuwa peke yake, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano(m.10).

Andiko

siku 12siku 14

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/2025

Soma Biblia Kila Siku 01/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Januari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko na Ezra. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz