Soma Biblia Kila Siku 11/2024Mfano
![Soma Biblia Kila Siku 11/2024](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F52667%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Yesu anatufundisha juu ya ndoa. Je, tutakubali kufuata neno lake? Daima ni baraka kwetu kulitii neno lake la ukweli. Wanafunzi waliguswa, wakawa na hofu. Maana wakati ule Wayahudi walijiona kuwa na uhuru sana katika masuala ya ndoa. Je, hata Watanzania wanajiona hivyo? Yesu anamikazo mitatu:1.Kufunga ndoa ni jambo jema lenye baraka. Ni mapenzi ya Mungu.2.Uaminifu mpaka kufa ni msingi wa ndoa.3.Kufunga ndoa zaidi ya mara moja haina kibali mbele ya Mungu. Kwa hiyo haiwezi kubarikiwa kanisani.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku 11/2024](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F52667%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz