Soma Biblia Kila Siku 11/2024Mfano
![Soma Biblia Kila Siku 11/2024](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F52667%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Leo jambo kuu ni hili: kuingia Mbinguni ni kwa neema tu. Ujira wetu, yaani uzima wa milele, ni uleule mmoja kwa wote, na hautolewi kutokana na ustahili wetu, bali kwa sababu Mungu ni mwema. Wanafunzi waliuliza,Tutapata nini basi(19:27)?Kwa hadithi hii Yesu anatuonya kwamba hata kama tumemtumikia kwa miaka mingi kwa uaminifu tusiwe tunaanza kujivuna na kufikiri tunastahili kuliko wengine. Tusiwaonee wivu waliochelewa kumpokea Yesu, bali tufurahi kwa sababu sisi wenyewe tumeokolewa:Msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni! (Lk 10:20)
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku 11/2024](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F52667%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku 11/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Kumi na moja pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz