Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 09/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 09/2024

SIKU 27 YA 30

Yehoahazi alitawala katika Israeli kwa kufuata utamaduni wa kidini wa Yeroboamu. Bwana hakupendezwa na Israeli, akawapa Hazaeli na Ben-Hadadi wa Shamu kuwapiga Israeli. Hatimaye Yehoahazi alikubali kumtafuta Bwana, na Bwana akamsikiliza na kuwapa mwokozi. “Kukaa hemani” (m.5) ni neno la mfano kwa kukaa kwa amani. Lakini inaonekana kwamba Yehoashi, mwana wa Yehoahazi, hakujali msaada huo, maana alifanya maovu.Hakuyaacha makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli; lakini akaendelea katika hayo(m.11). Je, shukrani zako kwa msaada wa Mungu zinaonekana katika unavyoishi?

siku 26siku 28

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 09/2024

Soma Biblia Kila Siku 09/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Tisa pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Mathayo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz

Mipangilio yanayo husiana