Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 08/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 08/2024

SIKU 1 YA 31

Wakati wa utawala wa Manase na Amoni, kipindi cha miaka 57 hivi, kilizaliwa kizazi ambacho hakikujua sheria ambazo Musa alipewa na Mungu kwa ajili ya taifa la Israeli. Mfalme Yosia aliporuhusu kazi ya kurekebisha hekalu ianze, ndipo mafundi wakakiona kitabu cha torati kilichohifadhiwa humo. Kwa Yosia, ambaye alimcha Bwana, hii ilikuwa habari njema kuwashirikisha watu. Tukimtumikia, Mungu aweza kutuonesha mambo mazuri ya sirini, lakini pia mambo ya kutisha. Hapa tunahitaji kutafakari sana m.13:Enendeni, mkamwulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu hawa, na kwa ajili ya Yuda yote, katika habari za maneno ya kitabu hiki kilichoonekana; kwa kuwa hasira ya Bwana ni kubwa aliyotukasirikia, kwa sababu baba zetu hawakuyaangalia maneno ya kitabu hiki, kufanya kama hayo yote tuliyoandikiwa.

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 08/2024

Soma Biblia Kila Siku 08/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Nane pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Wafalme na 1 Timotheo. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa maelezo zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz