Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

SIKU 26 YA 28

Kumbe, hata kama kizazi chetu tumemkosea Mungu, yeye anaweza kubadilisha mambo, tukapata kizazi kipya chenye kumpenda na kumwabudu Mungu. Ndivyo ilivyotokea Yuda, hata bila Abiya kutubu na kumwombea mtoto wake. Asa anaamua kufuata kama alivyofanya babaye Daudi. Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake (11-13). Matokeo yake, anapata kibali kwa Mungu, uongozi wake unabarikiwa, na jamii inafurahia matunda ya uongozi bora. Tutumie nafasi tuliyo nayo kwa ajili ya kumtumikia Mungu kwa uaminifu, naye atabariki na kuyafanikisha maisha yetu.

siku 25siku 27

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/