Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023Mfano

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

SIKU 20 YA 28

Mungu akiagiza jambo analifuatilia pia. Hivyo, ukiweka nadhiri kwa Mungu ni vizuri ukiitimiza. Pia jifunze kuisikiliza na kuitofautisha sauti ya Mungu na sauti zidanganyazo. Kwa mfano, mara nyingi ukifunga kwa maombi, utasikia sauti zinakushauri ule kidogo kwa siri. Hiyo siyo sauti ya Mungu. Mkristo, unapopewa rushwa utasikia sauti inasema hii ni shukrani tuu. Unafikiri hiyo ni sauti ya Mungu? Usidanganywe na roho hizo! Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani (1Tim. 4:1). Ulizingatie onyo hili ili usidanganyike.

siku 19siku 21

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku/ FEBRUARI 2023

Soma Biblia Kila Siku/Februari 2023 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo machache ya kukusaidia kuelewa zaidi neno ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Warumi na 1 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu bure

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/