Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F33529%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Nawaambia, hata katika Israeli sijaona imani kubwa namna hii (m.9). Jeshi la Warumi lilikuwa na kituo kikubwa hapo Kapernaumu na huyu bwana alikuwa ni jemadari (‘akida’). Ni mwenye cheo kikubwa maana aliweza kuwajengea Wayahudi sinagogi. Ndiyo maana wanamwambia Yesu wakisema, Amestahili huyu umtendee neno hili; maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi (m.4-5). Inaonekana kwamba alimwamini Mungu wa Wayahudi, maana kama m.5 unavyoonyesha, aliwapenda. Na imani yake ilikuwa ya kweli maana alimtambua Yesu na ukuu wake: sema neno tu (m.7). Ingawa ni mheshimwa sana katika mji huo alijiona si kitu mbele ya Yesu: sistahili. Omba uone zaidi ukuu wa Yesu!
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F33529%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Oktoba pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma k...
More
http://www.somabiblia.or.tz