Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Januari/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F29514%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Yakobo akaondoka, akapandisha wanawe na wakeze juu ya ngamia ... ili afike kwa Isaka babaye katika nchi ya Kanaani ... akamhadaa Labani, Mshami, kwa kuwa hakumwambia ya kwamba anakimbia (m.17-18 na 20). "Kumhadaa" maana yake ni kumdanganya au kumfanyia ujanja. Ilikuwa hatua ngumu sana kwa Yakobo. Tusisahau kwamba Labani ni mjomba wake! Lakini alipata nguvu na ujasiri, maana Mungu mwenyewe alimwagiza kuondoka (m.3 na 13, Bwana akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe … Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile uliyozaliwa). Tena Lea na Raheli wakamwunga mkono (m.14-16, Raheli na Lea wakajibu, wakamwambia, Je! Imetubakia sehemu au urithi katika nyumba ya baba yetu? Hakutufanya kama wageni, maana ametuuza, naye amekula fedha zetu kabisa? … Basi yo yote Mungu aliyokuambia, uyafanye)!
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Januari/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F29514%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/