Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 12Mfano

Soma Biblia Kila Siku 12

SIKU 17 YA 31

Neema huenda sambamba na haki ya Mungu. Hiyo huthibitishwa kwa namna mbili wakati waumini wakiteswa kwa ajili ya Yesu: 1. Mungu ana haki, akiwapa raha na utukufu pamoja na Yesu. Wastahili ufalme wake, si kwa sababu ya kuvumilia kwao, bali kwa sababu saburi yao huthibitisha imani yao kwamba i hai. 2. Mungu ana haki, akiwahukumu wale waliowaudhi waumini, maana tendo hilo huthibitisha uovu wao. Maangamizi yao ni sawa na kutengwa milele na Mungu mwenyewe, baraka zake na neema yake (m.8-9:Wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu … [wataadhibiwa] kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake). Yesu mwenyewe ataitekeleza hukumu hiyo, akija.

siku 16siku 18

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 12 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Mwanzo, Mathayo, 2 Wathesalonike na Zaburi.

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz