Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 12Mfano

Soma Biblia Kila Siku 12

SIKU 11 YA 31

Yesu analinganisha kurudi kwake na mwizi anavyoingia katika nyumba. Mwizi huingia kwa mtu saa asiyojua na hutenda uharibifu wa kusikitisha. Kwa Wakristo wote, hiki ni kielelezo kizuri kuonyesha inavyotupasa kukesha tukimngoja Bwana wetu. Kuna hatari ya sisi kukutwa tumelala arudipo Bwana wetu. Epuka hasara ya kukutwa umelala na Bwana wako. Fanya kama walinzi wafanyavyo! Wao wanajua kuwa kukaa macho, kusikiliza na kuchunguza kila tendo lenye mashaka maishani ndiyo njia ya kujiepusha na hasara.

siku 10siku 12

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 12 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Mwanzo, Mathayo, 2 Wathesalonike na Zaburi.

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz