Soma Biblia Kila Siku 4Mfano
![Soma Biblia Kila Siku 4](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F14800%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
"Eloi, Eloi, lama sabakthani?"Ndivyo Yesu alivyolia msalabani (Mt 27:46). Ni maneno ya kwanza ya somo la leo. Mwimba Zaburi alijisikia ameachwa na Mungu. Hata hivyo aliendelea kumtegemea. Hivyo ni mfano wa Yesu aliyesikia uchungu usiopimika wa kuachwa na Mungu alipobeba dhambi ya ulimwengu. Angalia kuwa wale waliomdhihaki Yesu walinukuu m.8. Maana katika Mt 27:43 imeandikwa: Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu. Mungu hakumponya Yesu, maana alitaka kuupatanisha ulimwengu na nafsi yake kwa njia ya kifo chake. Mungu asifiwe, maana awaokoa wote wamtumainiao.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku 4](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F14800%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku 4 inakupa mpango wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu, hasa kutoka Kitabu cha Kutoka, na 1 Wathesalonike, pamoja na maelezo juu ya somo hilo.
More
Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz