Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 4Mfano

Soma Biblia Kila Siku 4

SIKU 12 YA 30

Mungu aliwaongoza Waisraeli kwa njia ya pekee. Hakuchagua ile ya kawaida, ile ya Wafilisti, ingawa ilikuwa ya karibu, bali aliwaelekeza jangwani. Soma sababu katika m.17! Sisi sasa tunaelewa malengo ya Bwana kwao siku zile, lakini kuhusu njia za Bwana maishani mwetu, mara nyingi hatuelewi kama vile hao hawakuelewa kwanza. Ndipo tukumbuke kuwa yeye anajua kuliko sisi, na anatupenda. Inaonekana kwa jinsi Mungu alivyowaelekeza jangwani akiwa karibu nao na kuwaongoza wakati wote kwa njia ya nguzo ya wingu na ya moto. Pia sisi tunaomcha Bwana, tunaongozwa naye: Ni nani amchaye Bwana? Atamfundisha katika njia anayoichagua(Zab 25:12)!

siku 11siku 13

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 4

Soma Biblia Kila Siku 4 inakupa mpango wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu, hasa kutoka Kitabu cha Kutoka, na 1 Wathesalonike, pamoja na maelezo juu ya somo hilo.

More

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz