Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 01/2025Mfano

Soma Biblia Kila Siku 01/2025

SIKU 23 YA 31

Ujenzi wa nyumba ya Bwana unaanza kupata upinzani. Maadui wa Yuda na Benjamin wanaomba kushiriki katika ujenzi wa nyumba ya Bwana: Wakamkaribia Zerubabeli, na wakuu wa mbari za mababa, wakawaambia, Na tujenge sisi nasi pamoja nanyi; kwa maana tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi, nasi twamtolea dhabihu tangu zamani za Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru, aliyetupandisha mpaka hapa(m.2). Lakini walikataliwa kwa sababu Yuda walisema watu wa Mungu tu ndio walioamriwa kujenga na Mfalme Koreshi. Hapa tunaona viongozi wa watu wa Yuda wakiwa namsimamo. Kwa kutaka urahisi katika kutenda kazi ya Bwana tunaweza kuiharibu. Je, ni mara ngapi katika makanisa yetu tumefanya harambee na kualika watu ambao sio Wakristo ili mradi tu tupate fedha?

siku 22siku 24

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/2025

Soma Biblia Kila Siku 01/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Januari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko na Ezra. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz