Soma Biblia Kila Siku 02/20Mfano

Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi? (m.11) Swali hili liliulizwa na Mafarisayo walipoona Yesu ameketi nyumbani kwa Mathayo pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi. Baadaye huyu Mathayo akawa mtume, na ndiye aliyeiandika Injili hii tusomayo. Yesu alijibu swali, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi. Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi(m.12-13)! Yesu hakula nao ili kushirikiana nao katika maovu yao, bali kwa sababu aliwapenda. Ni wenye thamani kubwa kwa Mungu. Kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu(Lk 15:7). Alitaka awaokoe. Je, sisi Wakristo tunawapenda wasiomjua Mungu?
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 02/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo na Esta. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Kuwa Karibu Na Mungu Kila Siku

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Moyo - Neno La Mungu Hugeuza Moyo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Upendo Wa Bure
