Soma Biblia Kila Siku 12Mfano

Hekalu ilikuwa fahari ya Wayahudi. Liliashiria uhusiano wao na Mungu, na ndani yake walionana na Mungu. Wanafunzi walilionea shauku. Lakini Yesu alitabiri kuwa siku moja lingebomolewa; na lilibomolewa mwaka 70 b.K. Pia Bwana alitumia nafasi hii kueleza dalili za nyakati za mwisho. Je, umegundua dalili kuu na ndogo za kurudi kwa Yesu mara ya pili katika somo la leo? Tunaposoma na kuona dhahiri dalili hizi zinapotimia, hatuna budi kujiandaa kwa kurudi kwake, tukidumu ndani ya imani katika Yesu Kristo. Katika Yn 15:5-7 Yesu anatuambia inavyowezekana: Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea. Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 12 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Mwanzo, Mathayo, 2 Wathesalonike na Zaburi.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Kuwa Karibu Na Mungu Kila Siku

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku 02/20

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Upendo Wa Bure

SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20

Roho Mtakatifu - Tuna Uwezo Wa Kuwaka Moto Au La?
