Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 10Mfano

Soma Biblia Kila Siku 10

SIKU 3 YA 31

Mungu alijua kwamba sisi wanadamu hatuwezi wenyewe kusafisha maisha yetu. Hatuna haki wala utakatifu unaotustahilisha kuingia Mbinguni na kusimama mbele ya Mungu Mtakatifu! Aliona tumepotea. Ndipo akaamua kwa upendo wake kufanya upatanisho kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo ili tusafishwe katika damu yake. Kazi hii ya wokovu ni kazi aliyoifanya Mungu peke yake. Hapakuwa na ustahili wowote kwetu uliomfanya atende hivyo. Sababu ni moja tu: upendo wake! Zingatia m.8-10:Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake. Fungua moyo wako leo, umpokee Yesu!

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz