Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 59:10-17

Zaburi 59:10-17 BHN

Mungu wangu utanijia na fadhili zako, utaniwezesha kuwaona maadui zangu wameshindwa. Usiwaue mara moja, watu wangu wasije wakasahau; ila uwayumbishe kwa nguvu yako, uwaporomoshe chini. Ee Bwana, wewe ndiwe ngao yetu! Wao hutenda dhambi kwa yote wasemayo, kwa hiyo na wanaswe katika kiburi chao! Kwa sababu ya laana na uongo wao, uwateketeze kwa hasira yako, uwateketeze wasiwepo tena; ili watu wote wajue kuwa wewe ee Mungu watawala wazawa wa Yakobo hata mpaka miisho ya dunia. Kila jioni maadui hao hurudi wakibweka kama mbwa, na kuzungukazunguka mjini. Hupitapita huko na huko wakitafuta mlo, na wasipotoshelezwa hunguruma. Lakini mimi nitaimba sifa za nguvu yako; nitashangilia asubuhi juu ya fadhili zako; maana wewe umekuwa ngome yangu na kimbilio langu wakati wa taabu. Ewe uliye nguvu yangu, nitakuimbia sifa; ee Mungu, wewe u ngome yangu; Mungu mwenye kunifadhili!

Soma Zaburi 59