Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 59:10-17

Zaburi 59:10-17 NENO

Mungu wangu unayenipenda. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia. Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini. Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka, wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala katika Yakobo. Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji. Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa. Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida. Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unayenipenda.