Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 34:1-10

Zaburi 34:1-10 SRUV

Nitamhimidi BWANA kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima. Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie na kufurahi. Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja. Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa kutoka kwa hofu zangu zote. Mwelekezeeni macho, mpate kufurahi, Na nyuso zenu hazitaaibishwa kamwe. Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote. Malaika wa BWANA huwazungukia, Wamchao na kuwaokoa. Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumainia. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake, Maana, wamchao hawapungukiwi kitu. Wanasimba hutindikiwa, na kuona njaa; Bali wamtafutao BWANA hawapungukiwi kitu chochote kilicho chema.

Soma Zaburi 34

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 34:1-10