Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 34:1-10

Zaburi 34:1-10 NEN

Nitamtukuza BWANA nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote. Nafsi yangu itajisifu katika BWANA, walioonewa watasikia na wafurahi. Mtukuzeni BWANA pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja. Nilimtafuta BWANA naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote. Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe. Maskini huyu alimwita BWANA, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote. Malaika wa BWANA hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa. Onjeni mwone kwamba BWANA ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia. Mcheni BWANA enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote. Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao BWANA hawatakosa kitu chochote kilicho chema.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 34:1-10

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha