Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 34:1-10

Zab 34:1-10 SUV

Nitamhimidi BWANA kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima. Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja. Nalimtafuta BWANA akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote. Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya. Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote. Malaika wa BWANA hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa. Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake, Yaani, wamchao hawahitaji kitu. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao BWANA hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.

Soma Zab 34

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zab 34:1-10

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha