Zaburi 13:1-6
Zaburi 13:1-6 SRUV
Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele? Hadi lini utanificha uso wako? Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini? Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti. Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa. Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. Naam, nitamwimbia BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.