Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 13:1-6

Zaburi 13:1-6 NEN

Mpaka lini, Ee BWANA? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako mpaka lini? Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini? Nitazame, unijibu, Ee BWANA Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti. Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka. Lakini ninategemea upendo wako usiokoma; moyo wangu unashangilia katika wokovu wako. Nitamwimbia BWANA, kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 13:1-6

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha