Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele? Hadi lini utanificha uso wako? Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini? Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti. Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa. Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. Naam, nitamwimbia BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.
Soma Zaburi 13
Shirikisha
Linganisha Matoleo Yote: Zaburi 13:1-6
Hifadhi mistari, soma bila mtandao, tazama klipu za mafunzo, na zaidi!
YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video