Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 13:1-6

Zaburi 13:1-6 SRUV

Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele? Hadi lini utanificha uso wako? Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini? Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti. Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa. Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. Naam, nitamwimbia BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Soma Zaburi 13

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 13:1-6

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha