Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 13

13
Sala ya ukombozi kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 # Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2 Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele?
Hadi lini utanificha uso wako?
2Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini,
Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?
Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?
3 # Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14 Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;
Uyatie nuru macho yangu,
Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;
Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5 # 2 Nya 20:12 Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako;
Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6Naam, nitamwimbia BWANA,
Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 13: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha