Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 12

12
Ombi la msaada wakati wa dhiki
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata Sheminithi. Zaburi ya Daudi.
1 # Isa 57:1 Tuokoe, ee BWANA, maana hamna tena amchaye Mungu
Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
2Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,
Wenye midomo ya kujipendekeza;
Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
3BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,
Na ulimi unenao maneno ya kiburi;
4Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;
Midomo yetu ni yetu wenyewe,
Ni nani aliye bwana juu yetu?
5 # Kut 3:7,8 Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,
Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,
Sasa nitasimama, asema BWANA,
Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
6 # 2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5 Maneno ya BWANA ni maneno safi,
Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi;
Iliyosafishwa mara saba.
7Wewe, BWANA, ndiwe utakayetuhifadhi,
Utatulinda na kizazi hiki milele.
8Wasio haki hutembea pande zote,
Huku ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 12: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha