Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 13:1-6

Zab 13:1-6 SUV

Ee BWANA, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako? Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu? Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti. Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa. Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. Naam, nimwimbie BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Soma Zab 13

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zab 13:1-6

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha