Mwenyezi Mungu, Mungu wako, atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, yenye miji inayopendeza ambayo hukuijenga, nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba, jihadhari usije ukamwacha Mwenyezi Mungu, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.