Soma Biblia Kila Siku 8Sample
Kama ilivyokuwa upande wa baraka, ndivyo ilivyo upande wa laana pia. Ziko mikononi mwa Bwana, na atazileta usipotaka kuisikia sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake (m.15). M.16-29 inasema kuwa laana zitamfuata yeyote popote atakapokuwapo kama asipoisikia sauti ya Bwana. Angalia manano mazito yafuatayo, BWANA atakuletea laana … BWANA atakuambatanisha na tauni … BWANA atakupiga … BWANA atakufanya … (m.20-29). SALA: ”Bwana, usituingize kamwe chini ya laana zako”.
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku 8 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku hasa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Kumbukumbu la Torati, na Yohana pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More