YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 8Sample

Soma Biblia Kila Siku 8

DAY 14 OF 31

Waisraeli wote wamejumlishwa kwenye agano lake Mungu, wamo chini ya baraka au laana zake. Mtu asijidanganye kwa kuiendea miungu mingine akidai kuwa hakuna shida kwa kuwa yumo ndani ya agano la amani. Hakika ataonja laana zake Bwana (m. 18-21: Asiwe mtu katikati yenu ... ageukaye moyo wake leo amwache Bwana, Mungu wetu, kwenda kuitumikia miungu ya mataifa hayo; lisiwe katikati yenu shina lizaalo uchungu na pakanga; ikawa asikiapo maneno ya laana hii, ajibarikie mtu huyo moyoni mwake, na kusema, Nitakuwa katika amani, nijapotembea katika upotoe wa moyo wangu kwa kuangamiza mbichi na kavu; Bwana hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya Bwana na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na Bwana atalifuta jina lake chini ya mbingu. Bwana atamtenga kwa uovu, kutoka kabila zote za Israeli, kwa laana zote za agano lililoandikwa katika chuo hiki cha torati). Na vizazi vijavyo vitakapouliza kwa nini taifa la Israeli lilipelekwa kifungoni, jibu ni, Ni kwa kuwa waliacha agano la BWANA, … wakaenda wakatumikia miungu mingine (m.24-26). Hata leo linamchukiza sana Mungu mtu akimwacha na kutegemea miungu batili. 

Day 13Day 15