Soma Biblia Kila Siku 6Sample

Maana alikuwa ana nadhiri (m.18b). Paulo ni Myahudi na wakati fulani alifuata desturi za Kiyahudi zilizofundishwa na Musa (k.m. 21:26, Siku ya pili yake akajitakasa nafsi yake pamoja nao, akaingia ndani ya hekalu, akitangaza habari ya kutimiza siku za utakaso, hata sadaka itolewe kwa ajili ya kila mmoja wao). Kama ukitaka kufahamu zaidi kuhusu tendo la kutoa nadhiri (ahadi), unaweza kusoma Hesabu 6:1-21. Mstari wa 5 wasema: Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake sikue ziwe ndefu. Kuhusu umuhimu wa kazi ya Apolo huko Korintho (eneo la Akaya, m.27), tafakari ilivyoandikwa katika 1 Wakorintho 3:4-9,Hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa.Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe.Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Related Plans

Lead Through Prayer

Peace on Earth: A 5-Day Advent Devotional

Lift Others Up: 3 Days of Encouragement

Acts 18:24-19:22 | You Don't Need to Know It All

EquipHer Vol. 23: "Living With Intentionality"

The Wonder of the Wilderness

When God Is Silent: Finding Faith in the Waiting

From Choke Point to Calling: Finding Freedom With Jesus

Lead With Purpose: Kingdom Principles for Entrepreneurs
